Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mithali 15

15
1Jawabu la upole hugeuza hasira;
Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.
2Ulimi wa mwenye hekima hutamka maarifa vizuri;
Bali vinywa vya wapumbavu humwaga upumbavu.
3 # 2 Nya 16:9; Ayu 34:21; Mit 5:21; Yer 16:17; Zek 4:10; Ebr 4:13 Macho ya BWANA yako kila mahali;
Yakimchunguza mbaya na mwema.
4Ulimi safi ni mti wa uzima;
Bali ukorofi wa ulimi huvunja moyo.
5Mpumbavu hudharau kurudiwa na babaye;
Bali yeye aangaliaye maonyo hupata busara.
6Katika nyumba ya mwenye haki mna akiba nyingi;
Bali mapato ya mtu mbaya huwa taabu tu.
7Midomo ya mwenye haki hueneza maarifa;
Bali moyo wa mpumbavu haufanyi hivyo.
8 # Isa 61:8; Yer 6:20; Amo 5:22; Lk 18:11 Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;
Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake.
9 # Mit 21:21; Isa 51:1,7; 1 Tim 6:11 Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA;
Bali humpenda mtu afuatiaye wema.
10Adhabu kali ina yeye aiachaye njia;
Naye achukiaye kukemewa atakufa.
11 # Yn 2:24; Mdo 1:24 Kuzimu na Uharibifu viko wazi mbele za BWANA;
Si zaidi basi, mioyo ya wanadamu?
12Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa;
Wala yeye hawaendei wenye hekima.
13Moyo wa furaha huchangamsha uso;
Bali kwa huzuni ya moyo roho hupondeka.
14Moyo wa mwenye ufahamu hutafuta maarifa;
Bali kinywa cha wapumbavu hula upumbavu.
15Siku zote za mtu ateswaye ni mbaya;
Bali ukunjufu wa moyo ni karamu ya daima.
16 # Mit 16:8; Mhu 4:6; 1 Tim 6:6 Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA;
Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
17Chakula cha mboga palipo na upendo;
Ni bora kuliko ng'ombe aliyenona pamoja na kuchukiana.
18Mtu wa hasira huchochea ugomvi;
Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.
19Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba;
Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.
20Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye;
Bali mpumbavu humdharau mamaye.
21 # Efe 5:15 Upumbavu ni furaha kwake aliyepungukiwa na akili;
Bali mwenye ufahamu huunyosha mwenendo wake.
22Pasipo ushauri mipango vuhunjika;
Bali kwa wingi wa washauri huthibitika.
23Mtu hulifurahia jibu la kinywa chake;
Na neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!
24 # Flp 3:20 Kwa mtu mwenye akili njia ya uhai huenda juu;
Ili atoke katika kuzimu chini.
25BWANA ataing'oa nyumba ya mwenye kiburi;
Bali atauthibitisha mpaka wa mjane.
26Ushauri mbaya ni chukizo kwa BWANA;
Bali maneno yapendezayo ni safi.
27 # Yos 6:18; 1 Sam 8:3; Mit 1:19; Isa 5:8; Zek 5:3 Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;
Bali achukiaye zawadi ataishi.
28 # 1 Pet 3:15 Moyo wa mwenye haki hufikiri jinsi atakavyojibu;
Bali kinywa cha wasio haki humwaga mabaya.
29 # Efe 2:12; Zab 34:15,16; Yn 9:31; Rum 8:26 BWANA yuko mbali na wasio haki;
Bali huisikia sala ya mwenye haki.
30Mng'ao wa macho huufurahisha moyo;
Habari njema huinenepesha mifupa.
31Sikio lisikilizalo lawama yenye uhai
Litakaa kati yao wenye hekima.
32Akataaye maonyo huidharau nafsi yake mwenyewe;
Bali yeye asikilizaye lawama hujipatia ufahamu.
33Kumcha BWANA ni maonyo ya hekima;
Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.

Iliyochaguliwa sasa

Mithali 15: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha