Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hesabu 11

11
Manung'uniko katika jangwa
1 # Kut 15:23,24; 16:2,3,7,9; Kum 9:22; Omb 3:39; Law 10:2; 2 Fal 1:12 Kisha hao watu walikuwa kama wanung'unikao, wakinena maovu masikioni mwa BWANA; BWANA aliposikia hayo, hasira zake zikawaka; na moto wa BWANA ukawaka kati yao, ukateketeza hadi viunga vya kambi. 2#Yak 5:16 Ndipo watu wakamlilia Musa; naye Musa akamwomba BWANA, na ule moto ukakoma. 3Jina la mahali hapo likaitwa Tabera#11:3 Katika Kiebrania ni ‘kuchoma’. kwa sababu huo moto wa BWANA ukawaka kati yao.
4 # Kut 12:38; 1 Kor 10:6 Kisha mkutano wa wafuasi waliokuwa kati yao, wakashikwa na tamaa; wana wa Israeli nao wakalia tena, wakasema, Ni nani atakayetupa nyama tule? 5#Kut 16:3; Flp 3:19; Mt 6:24-34; Rum 8:7 Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu; 6lakini sasa roho zetu zimekauka; hakuna kitu chochote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hii mana tu. 7#Kut 16:31; Mwa 2:12 Na hiyo mana ilikuwa mfano wa chembe za mtama na rangi yake ilikuwa kama ya Bedola. 8Watu wakazungukazunguka na kuikusanya, kisha wakaisaga kwa mawe ya kusagia, au kuitwanga katika vinu, kisha wakaitokosa vyunguni na kuandaa mikate; na ladha yake ilikuwa kama ladha ya mafuta mapya. 9#Kut 16:13-15 Umande ulipoiangukia kambi wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao. 10Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za BWANA zikawaka sana; Musa naye akakasirika. 11#Kut 17:4; Kum 1:12; Yer 15:10,18; Yer 20:7-18; Mal 3:14; 2 Kor 11:28 Musa akamwambia BWANA, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu? 12#Isa 40:11; Eze 34:23; Yn 10:11; Isa 49:23; 1 The 2:7; Mwa 22:16; 26:3; Kut 13:5 Je! Ni mimi niliyewatungisha mimba watu hawa wote je! Ni mimi niliyewazaa, hata ikawa wewe kuniambia, Haya, wachukue kifuani mwako, mfano wa baba mwenye kulea achukuavyo mtoto anyonyaye, uende nao mpaka nchi uliyowaapia baba zao? 13#2 Fal 4:43; Mt 15:33; Mk 8:4 Nipate wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? Kwa nini wanililia, wakisema Tupe nyama, tupate kula. 14#Kut 18:18 Mimi siwezi kuwawaongoza watu hawa wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda. 15#1 Fal 19:4; Ayu 6:8-10; Yon 4:3; Sef 3:15 Na kama ukinitenda hivi, nakuomba uniulie mbali, ikiwa nimepata fadhili mbele ya macho yako; nami nisiyaone haya mashaka yangu.
Wazee sabini
16 # Kut 24:1,9 Kisha BWANA akamwambia Musa, Nikusanyie watu sabini, miongoni mwa wazee wa Israeli, ambao wewe unawajua kuwa ndio wazee wa watu hawa, na viongozi juu yao; ukawalete katika hema ya kukutania, wasimame huko pamoja nawe. 17#Mwa 11:5; Kut 19:20; 1 Sam 10:6; 2 Fal 2:5; Ayu 32:8; 38:36; Yoe 2:28 Nami nitashuka niseme nawe huko, nami nitatwaa sehemu ya roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao; nao watachukua mzigo wa watu hawa pamoja nawe, ili usiuchukue wewe peke yako. 18#Kut 19:10; 16:7; Mdo 7:39 Kisha uwaambie watu hawa, Jitakaseni nafsi zenu kabla ya kesho, nanyi mtakula nyama; kwa maana mmelia masikioni mwa BWANA, mkisema, Ni nani atakayetupa nyama, tule? Maana huko Misri tulikuwa na uheri. Basi kwa sababu hiyo BWANA atawapa nyama, nanyi mtakula. 19Hamtakula siku moja, wala siku mbili, wala siku tano, wala siku kumi, wala siku ishirini; 20lakini mtakula muda wa mwezi mzima, hadi hapo nyama hiyo itakapotoka katika mianzi ya pua zenu, nanyi mtaikinai, kwa sababu mmemkataa BWANA aliye kati yenu, na kulia mbele zake, mkisema, Tulitoka Misri kwa maana gani? 21Musa akasema, Watu hawa ambao mimi ni kati yao, ni watu elfu mia sita waendao kwa miguu; nawe umesema, Nitawapa nyama, ili wale muda wa mwezi mzima. 22#2 Fal 7:2; Mt 15:33; Mk 6:37 Je! Makundi ya kondoo na ng'ombe yatachinjwa kwa ajili yao, ili kuwatosha? Au samaki wote wa baharini watakusanywa pamoja kwa ajili yao, ili kuwatosha?
23 # Isa 50:2; Eze 12:25; 24:14 BWANA akamwambia Musa, Je! Mkono wa BWANA umepungua urefu wake?#11:23 Au ‘umekuwa mfupi kuliko ulivyokuwa’. Sasa utaona kama neno langu litatimizwa kwako, au la. 24Musa akatoka, akawaambia watu maneno ya BWANA; akawakutanisha watu sabini miongoni mwa wazee wa watu, akawaweka kuizunguka Hema. 25#Kut 34:5; 40:38; Hes 12:5; 2 Fal 2:15; 1 Sam 10:5,6; Yoe 2:29; Mdo 2:17,18; 1 Kor 14:1 Ndipo BWANA akashuka ndani ya wingu, akanena naye, akatwaa sehemu ya roho iliyokuwa juu ya Musa, akaitia juu ya wale wazee sabini; ikawa, roho hiyo ilipowashukia, wakatabiri, lakini hawakufanya hivyo tena. 26#1 Sam 20:26; Yer 36:5 Lakini watu wawili walisalia kambini, jina la mmoja aliitwa Eldadi, na jina la wa pili aliitwa Medadi; na roho ile ikawashukia; nao walikuwa miongoni mwao walioandikwa, lakini walikuwa hawakutoka kwenda hemani; nao wakatabiri kambini. 27Mtu mmoja kijana akapiga mbio, akaenda akamwambia Musa, akasema, Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini. 28#Mk 9:38; Yn 3:26 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa tangu ujana wake, akajibu akasema, Ee bwana wangu Musa, uwakataze. 29#Mdo 26:29; 1 Kor 14:5 Musa akamwambia, Je! Umekuwa na wivu kwa ajili yangu; ingekuwa heri kama watu wote wa BWANA wangekuwa manabii na kama BWANA angewatia roho yake. 30Kisha Musa akaenda akaingia kambini, yeye na wale wazee wa Israeli.
Kware
31 # Zab 78:26 Kisha upepo ukavuma kutoka kwa BWANA, nao ukaleta kware kutoka pande za baharini, nao ukawaacha wakaanguka karibu na kambi, kama kiasi cha mwendo wa siku moja upande huu, na kama kiasi cha mwendo wa siku moja upande ule, kuizunguka, nao wakafikia kiasi cha dhiraa mbili juu ya uso wa nchi. 32#Kut 16:36; Eze 45:11 Watu wakaondoka mchana huo wote, na usiku huo wote, na siku ya pili yote, kuwakusanya hao kware; yeye aliyepata ya upungufu kuliko wenziwe alipata kiasi cha homeri#11:32 Ni kama kilo elfu moja. kumi; nao wakawaanika wote kandokando ya kambi kuizunguka pande zote. 33#Zab 78:30; 106:14 Kisha hapo hiyo nyama ilipokuwa ikali kati ya meno yao, hawajaitafuna bado, hasira za BWANA ziliwaka juu ya watu, BWANA akawapiga watu kwa pigo kuu mno. 34#Kum 9:22 Jina la mahali pale likaitwa Kibroth-hataava;#11:34 Maana yake ni ‘Makaburi yatamea’. maana, ni hapo walipowazika hao watu waliotamani. 35#Hes 33:17; Kum 1:1 Kutoka hapo Kibroth-hataava watu wakasafiri kwenda Haserothi; wakakaa huko Haserothi.

Iliyochaguliwa sasa

Hesabu 11: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia