Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Malaki 1:1-5

Malaki 1:1-5 SRUV

Ufunuo wa neno la BWANA kwa Israeli kwa mkono wa Malaki Nimewapenda ninyi, asema BWANA. Lakini ninyi mwasema, Umetupendaje? Je! Esau siye ndugu yake Yakobo? Asema BWANA; ila nimempenda Yakobo; bali Esau nimemchukia na kuifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa mbweha wa nyikani. Ijapokuwa Edomu asema, Tumepondwapondwa, lakini tutarudi na kupajenga mahali palipoachwa hali ya ukiwa; BWANA wa majeshi asema hivi, Wao watajenga, bali mimi nitaangusha; na watu watawaita, Mpaka wa uovu, na, Watu ambao BWANA anawaghadhabikia milele. Na macho yenu ninyi yataona, nanyi mtasema, BWANA ndiye mkuu hata katika nje ya mipaka ya Israeli.

Soma Malaki 1

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Malaki 1:1-5