Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 39

39
1Je! Wajua majira ya kuzaa kwao mbuzi-mwitu walio majabalini?
Au waweza kusema majira ya kuzaa kwa kulungu?
2Je! Waweza kuhesabu miezi yao watakayoitimiza?
Au waweza kusema majira ya kuzaa kwa kulungu?
3Wao hujiinamisha, kuzaa watoto wao,
Watupa taabu zao.
4Watoto wao wako katika hali nzuri, hukua katika bara wazi;
Huenda zao, wala hawarudi tena.
5Ni nani aliyemwacha pundamilia aende huru?
Au je! Ni nani aliyemfungulia vifungo punda mwitu?
6 # Ayu 24:5; Yer 2:24; Hos 8:9 Ambaye nimeifanya nyika kuwa nyumba yake,
Na nchi ya chumvi kuwa makao yake.
7Yeye hudharau mshindo wa mji,
Wala hasikii kelele zake msimamizi.
8Upana wa milima ni malisho yake,
Hutafutatafuta kila kitu kilicho kibichi.
9Je! Nyati atakubali kukutumikia?
Au atakaa katika zizi lako?
10Je! Waweza kumfunga nyati kwa kamba matutani?
Au, yeye atayalima mabonde nyuma yako?
11Je! Utamtumaini kwa sababu ana nguvu nyingi?
Au, utamwachia yeye kazi yako?
12Je! Utamtumaini kwamba ataileta mbegu yako nyumbani.
Na kukusanya nafaka ya kiwanja chako cha kupuria?
13Bawa la mbuni hufurahi;
Lakini mabawa yake na manyoya yake, je! Yana huruma?
14Kwa maana yeye huyaacha mayai yake juu ya nchi,
Na kuyatia moto mchangani,
15Na kusahau kwamba huenda mguu ukayavunja,
Au mnyama-pori kuyakanyaga.
16 # Law 26:29; Isa 49:15; Yer 19:9; Omb 2:20; Eze 5:10 Yeye huwatendea ukatili makinda yake, kama kwamba si yake;
Ijapokuwa kazi yake yaweza kuwa ya bure, yeye hana hofu;
17 # Ayu 35:11 Kwa sababu Mungu amemnyima akili,
Wala hakumpa fahamu.
18Wakati anapojiinua juu aende,
Humdharau farasi na mwenye kumpanda.
19Je! Wewe ulimpa farasi uwezo wake?
Au, ni wewe uliyemvika shingo yake manyoya yatetemayo?
20Ndiwe uliyemfanya aruke kama nzige?
Fahari ya mlio wake hutisha.
21 # Yer 8:6 Huparapara bondeni, na kuzifurahia nguvu zake;
Hutoka kwenda kukutana na wenye silaha.
22Yeye hufanyia kicho dhihaka, wala hashangai;
Wala hageuki kurudi nyuma mbele ya upanga.
23Podo humpigia makelele,
Mkuki ung'aao na fumo.
24Huimeza nchi kwa ukali wake na ghadhabu;
Wala hasimami kwa sauti ya baragumu.
25Kila ipigwapo baragumu yeye husema, Aha!
Naye husikia harufu ya vita toka mbali,
Mshindo wa makamanda, na makelele.
26Je! Mwewe huruka juu kwa akili zako,
Na kuyanyosha mabawa yake kwenda kusini?
27 # Yer 49:16 Je! Tai hupaa juu kwa amri yako,
Na kufanya kiota chake mahali pa juu?
28Hukaa jabalini, ndiko kwenye malazi yake,
Juu ya genge la jabali, na ngomeni.
29Toka huko yeye huchungulia mawindo;
Macho yake huyaangalia toka mbali.
30 # Mt 24:28; Lk 17:37 Makinda yake nayo hufyonza damu;
Na pale iliko mizoga ndiko aliko.

Iliyochaguliwa sasa

Ayubu 39: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia