Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 35:30-35

Kutoka 35:30-35 SRUV

Kisha Musa akawaambia wana wa Israeli, Angalieni, BWANA amemwita kwa jina lake Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda; naye amemjaza Roho ya Mungu, katika hekima, na akili, na ujuzi, na kazi ya ustadi kila aina; na kuvumbua kazi za werevu, na kufanya kazi ya dhahabu, fedha na shaba, na kukata vito vya kutilia, na kuchora miti, atumike katika kazi za ufundi wa kila aina. Naye amemtilia moyoni mwake uwezo ili apate kufundisha, yeye, na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani. Amewajaza watu hao ujuzi, ili watumike katika kazi za kila aina, mawe, na kazi ya fundi mwenye kutia taraza, katika nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani nzuri, ya mwenye kufuma nguo; ya hao wafanyao kazi yoyote, na ya wenye kuvumbua kazi za werevu.

Soma Kutoka 35

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Kutoka 35:30-35