Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Matendo 3:4-9

Matendo 3:4-9 SRUV

Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi. Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao. Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende. Akamshika mkono wa kulia, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu. Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akirukaruka, na kumsifu Mungu. Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu.

Soma Matendo 3

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Matendo 3:4-9