Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Timotheo 1:8-11

1 Timotheo 1:8-11 SRUV

Lakini twajua ya kuwa sheria ni njema, kama mtu akiitumia kwa njia iliyo halali; akilifahamu neno hili, ya kuwa sheria haimhusu mtu asiye na hatia, bali wavunjao sheria, waasi, na makafiri, na wenye dhambi, na wanajisi, na wasiomcha Mungu, na wapigao baba zao, na wapigao mama zao, na wauaji, na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na linginelo lolote lisilopatana na mafundisho ya kweli; kama ilivyonenwa katika Habari Njema ya utukufu wa Mungu ahimidiwaye, niliyowekewa amana.