Zaburi 14
14
Kushutumiwa kwa wasiomwamini Mungu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 #
Rum 3:10-12; Zab 10:4; Mit 1:7,22; Mwa 6:12 Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu;
Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo,
Hakuna atendaye mema.
2Toka mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu,
Aone kama yuko mtu mwenye hekima,
Amtafutaye Mungu.
3Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja,
Hakuna atendaye mema,
La! Hata mmoja.
4Je! Wote wafanyao maovu hawajui?
Walao watu wangu kama walavyo mkate,
Hawamwiti BWANA.
5Hapo ndipo waovu watakaposhikwa na hofu nyingi,
Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.
6Mnaiharibu mipango ya mtu mnyonge,
Bali BWANA ndiye aliye kimbilio lake.
7Laiti wokovu wa Israeli ungetoka katika Sayuni!
BWANA awarudishapo wafungwa wa watu wake;
Yakobo atashangilia,
Israeli atafurahi.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 14: SRUVDC
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.