Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 130

130
Kusubiri Wokovu wa Mungu
Wimbo wa kupanda mlima.
1 # Omb 3:55; Yon 2:2 Ee BWANA, toka vilindini nimekulilia.
2Bwana, uisikie sauti yangu.
Masikio yako na yaisikilize
Sauti ya dua zangu.
3 # Zab 143:2; Yn 8:7-9; Rum 3:20 BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu,
Ee Bwana, nani angesimama?
4 # 2 The 1:6; Zab 37:2; Yer 17:6; Kut 3:4,7; Efe 1:7; 1 Fal 8:40; Yer 33:8,9; Ebr 12:28 Lakini kwako kuna msamaha,
Ili Wewe uogopwe.
5 # Isa 26:8 Nimemngoja BWANA, roho yangu imengoja,
Na neno lake nimelitumainia.
6Nafsi yangu inamngoja Bwana,
Kuliko walinzi waingojavyo asubuhi,
Naam, walinzi waingojao asubuhi.
7 # Isa 55:7 Ee Israeli, umtarajie BWANA;
Maana kwa BWANA kuna fadhili,
Na kwake kuna ukombozi mwingi.
8 # Mt 1:21; Tit 2:14 Yeye atamkomboa Israeli na maovu yake yote.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 130: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha