Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayu 12

12
Ayubu Ajibu: Mimi Nachekwa Sana
1Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2Hapana shaka ninyi ndinyi watu halisi,
Nanyi mtakapokufa, ndipo na hekima itakoma.
3Lakini mimi pia, nina fahamu kama ninyi;
Mimi si duni yenu ninyi;
Naam, ni nani asiyejua mambo kama hayo?
4 # Ayu 16:20; Zab 91:15; Yer 33:3; Mik 7:7 Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake,
Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu;
Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko.
5 # Mit 14:2 Katika mawazo yake huyo aliye na raha mna kudharau mashaka;
Tayari kwa ajili ya wenye kuteleza miguu.
6Hema za wapokonyi hufanikiwa,
Na hao wamkasirishao Mungu hukaa salama;
Mikononi mwao Mungu huleta vitu vingi.
7Lakini sasa waulize hao wanyama, nao watakufundisha;
Na nyuni wa angani, nao watakuambia;
8Au nena na nchi, nayo itakufundisha;
Nao samaki wa baharini watakutangazia.
9Katika hawa wote ni yupi asiyejua,
Kwamba ni mkono wa BWANA uliofanya haya?
10 # Hes 16:22; Dan 5:23; Mdo 17:28 Ambaye nafsi ya kila kilicho hai i mkononi mwake,
Na pumzi zao wanadamu wote.
11Je! Sikio silo lijaribulo maneno,
Kama vile kaakaa lionjavyo chakula?
12Wazee ndio walio na hekima,
Na katika kuishi siku nyingi iko fahamu.
13Hekima na amri zina yeye [Mungu];
Yeye anayo mashauri na fahamu.
14 # Ufu 3:7 Tazama, yuavunja, wala haiwezekani kujenga tena;
Humfunga mtu, wala haiwezekani kumfungua.
15 # 1 Fal 17:1; Mwa 7:11 Tazama, yuayazuia maji, nayo yakatika;
Tena, huyapeleka, nayo yaipindua dunia.
16Kwake yeye ziko nguvu, na makusudi kufanikiwa;
Huyo adanganywaye, na mdanganyi pia ni wake.
17Yeye huwaondoa washauri hali wametekwa nyara,
Naye huwafanya waamuzi kuwa ni wapumbavu.
18Yeye hulegeza kifungo cha wafalme,
Na kuwafunga viuno vyao kwa mshipi.
19Yeye huwaondoa makuhani hali wametekwa nyara.
Na kuwapindua mashujaa.
20Huondoa matamko ya hao walioaminiwa,
Na kuondoa fahamu za wazee.
21Humwaga aibu juu ya hao wakuu,
Na kulegeza mshipi wa wenye nguvu.
22 # Mt 10:26; 1 Kor 4:5 Huvumbua mambo ya siri tokea gizani,
Na hicho kilicho giza tupu huleta mwangani.
23Huyaongeza mataifa, na kuyaangamiza;
Huyaeneza mataifa mbali, na kuyaacha.
24Huwaondolea moyo wakuu wa watu wa nchi,
Na kuwapoteza nyikani pasipokuwa na njia.
25Wao hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga,
Naye huwafanya kupepesuka kama vile mlevi.

Iliyochaguliwa sasa

Ayu 12: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha