Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hab UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu hiki kinazungumzia suala la mateso, dhambi na haki ya Mungu kama ilivyo kwa Ayubu na Zaburi ya 73. Habakuki anaanza kwa kumlalamikia Mungu kuwa Yuda hakutekeleza ujumbe aliopewa. Anauliza, hadi lini Yuda waendelee katika uovu bila kuadhibiwa. Mungu anajibu kuwa anaandaa adhabu itakayotolewa kwa kutumia Wakaldayo (Wababeli). Habakuki anabisha mpango huo akisema: kama Mungu ni Mtakatifu na wa haki, na Wayahudi ni watu wake itawezekanaje Wakaldayo wenye maovu mengi kuliko Wayuda watumiwe na Mungu? Jibu la Mungu ni kuwa kila dhambi huleta hukumu. Hivyo wote watapata adhabu ya uovu wao.
Habakuki, ambaye maana yake ni “kumbatia” au “mshindani mweleka” haelezi maisha yake binafsi na hataji kwa uwazi mwaka alipotoa ujumbe. Ujumbe wenyewe unaelekeza kuwa ni wakati Wakaldayo (Wababeli) walipokuwa wakitawala Ashuru, Misri na Yuda lakini kabla ya kubomoa Yerusalemu.
Ujumbe wa Habakuki ni BWANA Mungu sio Mungu wa Israeli na Yuda tu, yeye ni Mungu wa ulimwengu wote. Yuda na Kaldayo (Babeli) wataadhibiwa kwa kufuata maovu yao. Vile vile amtegemeaye Mungu akawa mwadilifu hana haja ya kuogopa hukumu maana “Mwenye haki ataishi kwa Imani”. Mungu atampa ushindi (2:4).
Yaliyomo:
1. Malalamiko ya Habakuki na Jibu la Mungu, Sura 1:1–2:5
2. Uovu wa Wababeli, Sura 2:6-20
3. Sala ya Habakuki, Sura 3

Iliyochaguliwa sasa

Hab UTANGULIZI: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha