Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

2 Fal 8:7-13

2 Fal 8:7-13 SUV

Kisha, Elisha akaenda Dameski; na Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, alikuwa hawezi; akaambiwa ya kwamba, Yule mtu wa Mungu amefika hapa. Mfalme akamwambia Hazaeli, Chukua zawadi mkononi mwako, ukaende ili kumlaki yule mtu wa Mungu, ukamwulize BWANA kwa kinywa chake, kusema, Je! Nitapona ugonjwa huu? Basi Hazaeli akaenda kumlaki, akachukua zawadi mkononi mwake, za kila kitu chema kilichopatikana Dameski, kiasi cha mizigo ya ngamia arobaini, akaenda, akasimama mbele yake akasema, Mwana wako Ben-hadadi, mfalme wa Shamu, amenituma kwako, kusema, Je nitapona ugonjwa huu? Elisha akamwambia, Enenda, ukamwambie, Bila shaka utapona; lakini BWANA amenionyesha ya kwamba bila shaka atakufa. Akamkazia macho hata akatahayari; na yule mtu wa Mungu akalia machozi. Hazaeli akasema, Bwana wangu analilia nini? Akajibu, Kwa sababu nayajua mabaya utakayowatenda wana wa Israeli; utazichoma moto ngome zao, utawaua vijana wao kwa upanga, utawaseta-seta watoto wao wachanga na wanawake wao wenye mimba utawapasua. Hazaeli akasema, Lakini mimi mtumwa wako ni nani, mimi niliye mbwa tu, hata nifanye jambo hili kubwa? Elisha akajibu, BWANA amenionyesha ya kwamba wewe utakuwa mfalme juu ya Shamu.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na 2 Fal 8:7-13