Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

2 Fal 10:30-36

2 Fal 10:30-36 SUV

BWANA akamwambia Yehu, Kwa kuwa umetenda vema kwa kufanya vilivyo haki machoni pangu, kuitendea nyumba ya Ahabu sawasawa na yote yaliyomo moyoni mwangu, wana wako wa kizazi cha nne watakaa kitini mwa Israeli. Lakini Yehu hakuangalia, aende katika sheria ya BWANA, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote; hakutoka katika makosa ya Yeroboamu, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli. Siku zile BWANA akaanza kupunguza Israeli. Hazaeli akawapiga mipakani mwote mwa Israeli; kutoka Yordani upande wa mashariki, nchi yote ya Gileadi, na ya Wagadi, na Wareubeni, na Wamanase, kutoka Aroeri iliopo karibu na bonde la Arnoni, yaani, Gileadi, na Bashani. Basi mambo yote ya Yehu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na ushujaa wake, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli? Yehu akalala na babaze; wakamzika katika Samaria. Na Yehoahazi mwanawe akatawala mahali pake. Na muda Yehu aliotawala juu ya Israeli katika Samaria ulikuwa miaka ishirini na minane.

Soma 2 Fal 10

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na 2 Fal 10:30-36