Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Sefania 1:7-12

Sefania 1:7-12 NEN

Nyamazeni mbele za BWANA Mwenyezi, kwa maana siku ya BWANA iko karibu. BWANA ameandaa dhabihu, amewaweka wakfu wale aliowaalika. Katika siku ya dhabihu ya BWANA nitawaadhibu wakuu na wana wa mfalme na wale wote wanaovaa nguo za kigeni. Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao hukwepa kukanyaga kizingiti, ambao hujaza hekalu la miungu yao kwa dhuluma na udanganyifu.” BWANA asema, “Katika siku hiyo kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki, maombolezo kutoka mtaa wa pili, na mshindo mkubwa kutoka vilimani. Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni; wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa, wote ambao wanafanya biashara ya fedha wataangamizwa. Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa, na kuwaadhibu wale ambao wanakaa katika hali ya kuridhika, ambao ni kama divai iliyobaki kwenye machicha, ambao hudhani, ‘BWANA hatafanya lolote, jema au baya.’

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha