Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zekaria 1:1-6

Zekaria 1:1-6 NENO

Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Dario, neno la BWANA lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema: “BWANA aliwakasirikia sana baba zako wa zamani. Kwa hiyo waambie watu: Hili ndilo asemalo BWANA wa majeshi: ‘Nirudieni mimi,’ asema BWANA wa majeshi, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema BWANA wa majeshi. Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hili ndilo asemalo BWANA wa majeshi: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema BWANA. Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele? Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu? “Kisha walitubu na kusema, ‘BWANA wa majeshi ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’ ”