Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 91

91
Zaburi 91
Mwenyezi Mungu mlinzi wetu
1Yeye akaaye mahali pa salama pake Yeye Aliye Juu Sana,
atadumu katika uvuli wake Mwenyezi.#91:1 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania.
2Nitasema kumhusu Mwenyezi Mungu, “Yeye ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu, ninayemtumaini.”
3Hakika yeye ataniokoa na mtego wa mwindaji,
na maradhi ya kuambukiza ya kuua.
4Atakufunika kwa manyoya yake,
chini ya mabawa yake utapata kimbilio,
uaminifu wake utakuwa ngao na kinga yako.
5Hutaogopa vitisho vya usiku,
wala mshale urukao mchana,
6wala maradhi ya kuambukiza
yanayonyemelea gizani,
wala tauni iharibuyo adhuhuri.
7Ijapo watu elfu wataangukia kando yako,
kumi elfu mkono wako wa kuume,
lakini haitakukaribia wewe.
8Utatazama tu kwa macho yako
na kuona adhabu ya waovu.
9Ukimfanya Aliye Juu Sana kuwa makao yako;
naam, Mwenyezi Mungu ambaye ni kimbilio langu;
10basi hakuna madhara yatakayokupata wewe,
hakuna maafa yatalikaribia hema lako.
11Kwa kuwa atawaagiza malaika wake kwa ajili yako,
wakulinde katika njia zako zote.
12Watakuchukua mikononi mwao,
ili usijikwae mguu wako kwenye jiwe.
13Utawakanyaga simba na nyoka wakali,
simba mkubwa na nyoka utawaponda kwa miguu.
14Mwenyezi Mungu asema, “Kwa kuwa ananipenda, nitamwokoa;
nitamlinda, kwa kuwa analikiri Jina langu.
15Ataniita, nami nitamjibu;
nitakuwa pamoja naye katika taabu,
nitamwokoa na kumheshimu.
16Kwa siku nyingi nitamshibisha
na kumwonesha wokovu wangu.”

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 91: NENO

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia