Zaburi 79
79
Zaburi 79
Maombi kwa ajili ya wokovu wa taifa
Zaburi ya Asafu.
1Ee Mungu, mataifa yameuvamia urithi wako,
wamelinajisi Hekalu lako takatifu,
wameifanya Yerusalemu kuwa magofu.
2Wametoa maiti za watumishi
kuwa chakula cha ndege wa angani
na nyama ya watakatifu wako
kwa wanyama wa nchi.
3Wamemwaga damu kama maji
kuzunguka Yerusalemu yote,
wala hakuna yeyote wa kuwazika.
4Tumekuwa kitu cha aibu kwa majirani zetu,
cha dharau na mzaha kwa wale wanaotuzunguka.
5Hata lini, Ee Mwenyezi Mungu? Je, wewe utakasirika milele?
Wivu wako utawaka kama moto hadi lini?
6Mwaga ghadhabu yako kwa mataifa yasiyokukubali,
juu ya falme za hao wasioliitia jina lako,
7kwa maana wamemrarua Yakobo
na kuharibu nchi ya makao yake.
8Usituhesabie dhambi za baba zetu,
huruma yako na itujie hima,
kwa maana tu wahitaji mno.
9Ee Mungu Mwokozi wetu, utusaidie,
kwa ajili ya utukufu wa jina lako;
tuokoe na kutusamehe dhambi zetu
kwa ajili ya jina lako.
10Kwa nini mataifa waseme,
“Yuko wapi Mungu wenu?”
Mbele ya macho yetu,
dhihirisha kati ya mataifa
kwamba unalipiza kisasi damu iliyomwagwa
ya watumishi wako.
11Kilio cha huzuni cha wafungwa kifike mbele zako;
kwa nguvu za mkono wako
hifadhi wale waliohukumiwa kufa.
12Walipize majirani zetu mara saba
aibu walizovurumisha kwako, Ee Bwana.
13Ndipo sisi watu wako, kondoo wa malisho yako,
tutakusifu milele;
tutasimulia sifa zako
kizazi hadi kizazi.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 79: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.