Zaburi 47
47
Zaburi 47
Mtawala Mwenye Enzi Yote
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora.
1 Pigeni makofi, enyi mataifa yote,
mpigieni Mungu kelele za shangwe!
2 Jinsi gani alivyo wa kutisha, Bwana Aliye Juu Sana,
Mfalme mkuu juu ya dunia yote!
3 Ametiisha mataifa chini yetu
watu wengi chini ya miguu yetu.
4 Alituchagulia urithi wetu,
fahari ya Yakobo, aliyempenda.
5 Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,
Bwana kwa sauti za tarumbeta.
6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa,
mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.
7 Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote,
mwimbieni zaburi za sifa.
8 Mungu anatawala juu ya mataifa,
Mungu ameketi juu ya kiti chake cha enzi kitakatifu.
9 Wakuu wa mataifa wanakusanyika
kama watu wa Mungu wa Abrahamu,
kwa kuwa wafalme wa dunia ni mali ya Mungu;
yeye ametukuka sana.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 47: NEN
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™
Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Version™
Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 by Biblica, Inc.
Used with Permission. All Rights Reserved Worldwide.