Zaburi 40:1-4
Zaburi 40:1-4 NENO
Nilimngoja Mwenyezi Mungu kwa saburi, naye akanijia na kusikia kilio changu. Akanipandisha kutoka shimo la uharibifu, kutoka matope na utelezi; akaiweka miguu yangu juu ya mwamba na kunipa mahali imara pa kusimama. Akaweka wimbo mpya kinywani mwangu, wimbo wa sifa kwa Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa na kuweka tumaini lao kwa Mwenyezi Mungu. Heri mtu yule amfanyaye Mwenyezi Mungu kuwa tumaini lake, asiyewategemea wenye kiburi, wale wenye kugeukia miungu ya uongo.