Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 30:1-12

Zaburi 30:1-12 NEN

Nitakutukuza wewe, Ee BWANA, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu. Ee BWANA, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya. Ee BWANA, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. Mwimbieni BWANA, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu. Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha. Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.” Ee BWANA, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika. Kwako wewe, Ee BWANA, niliita, kwa Bwana niliomba rehema: “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako? Ee BWANA, unisikie na kunihurumia, Ee BWANA, uwe msaada wangu.” Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe, ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee BWANA Mungu wangu, nitakushukuru milele.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 30:1-12

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha