Zaburi 21
21
Zaburi 21
Shukrani kwa Mwenyezi Mungu kwa ajili ya ushindi
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1Ee Mwenyezi Mungu, mfalme huzifurahia nguvu zako.
Tazama jinsi furaha yake ilivyo kuu
kwa ushindi unaompa!
2Umempa haja ya moyo wake
na hukumzuilia maombi ya midomo yake.
3Ulimkaribisha kwa baraka tele
na kumvika taji la dhahabu safi kichwani pake.
4Alikuomba maisha, nawe ukampa,
wingi wa siku milele na milele.
5Kutokana na ushindi uliompa, utukufu wake ni mkubwa,
umeweka juu yake fahari na utukufu.
6Hakika umempa baraka za milele,
umemfanya awe na furaha
kwa shangwe ya uwepo wako.
7Kwa kuwa mfalme anamtumaini Mwenyezi Mungu;
kwa upendo usiokoma wa Aliye Juu Sana hatatikiswa.
8Mkono wako utawashika adui zako wote,
mkono wako wa kuume utawakamata adui zako.
9Wakati utajitokeza,
utawafanya kama tanuru la moto.
Katika ghadhabu yake Mwenyezi Mungu atawameza,
moto wake utawateketeza.
10Utawaangamiza wazao wao kutoka duniani,
uzao wao kutoka wanadamu.
11Ingawa watapanga mabaya dhidi yako
na kutunga hila, hawawezi kufanikiwa,
12kwa kuwa utawafanya wakimbie
utakapowalenga usoni pao
kwa mshale kutoka upinde wako.
13Ee Mwenyezi Mungu, utukuzwe katika nguvu zako,
tutaimba na kusifu nguvu zako.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 21: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.