Zaburi 16
16
Zaburi 16
Sala ya matumaini
Utenzi wa Daudi.
1Ee Mungu, uniweke salama,
kwa maana kwako nimekimbilia.
2Nilimwambia Mwenyezi Mungu, “Wewe ndiwe Bwana wangu;
pasipo wewe sina jambo jema.”
3Kuhusu watakatifu walio duniani,
hao ndio wenye fahari,
na ninapendezwa nao.
4Huzuni itaongezeka kwa wale
wanaokimbilia miungu mingine.
Sitazimimina sadaka za damu kwa miungu kama hiyo,
au kutaja majina yao mdomoni mwangu.
5Mwenyezi Mungu umeniwekea fungu langu na kikombe changu;
umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.
6Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,
hakika nimepata urithi mzuri.
7Nitamsifu Mwenyezi Mungu ambaye hunishauri,
hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.
8Nimemweka Mwenyezi Mungu mbele yangu daima.
Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume,
sitatikisika.
9Kwa hiyo moyo wangu unafurahia,
na ulimi wangu unashangilia;
mwili wangu nao
utapumzika salama,
10kwa maana hutaniacha Kuzimu#16:10 Kuzimu kwa Kiebrania ni Sheol, yaani Shimo lisilo na mwisho.,
wala hutamwacha Mtakatifu Wako
kuona uharibifu.
11Umenijulisha njia ya uzima;
utanijaza na furaha mbele zako,
pamoja na furaha ya milele
katika mkono wako wa kuume.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 16: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.