Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 14

14
Zaburi 14
Uovu Wa Wanadamu
(Zaburi 53)
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna hata mmoja atendaye mema.
2 Bwana anawachungulia wanadamu chini
kutoka mbinguni
aone kama wako wenye akili,
wowote wanaomtafuta Mungu.
3 Wote wamepotoka,
wameharibika wote pamoja,
hakuna atendaye mema.
Naam, hakuna hata mmoja!
4 Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwiti Bwana?
5Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu,
maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,
bali Bwana ndiye kimbilio lao.
7 Laiti wokovu wa Israeli
ungalikuja kutoka Sayuni!
Wakati Bwana arejeshapo
wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie,
Israeli na afurahi!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 14: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha