Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 130

130
Zaburi 130
Kuomba Msaada
Wimbo wa kwenda juu.
1 Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Ee Bwana, sikia sauti yangu.
Masikio yako na yawe masikivu
kwa kilio changu unihurumie.
3 Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,
Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 Lakini kwako kuna msamaha,
kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea,
katika neno lake naweka tumaini langu.
6 Nafsi yangu inamngojea Bwana
kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,
naam, kuliko walinzi
waingojeavyo asubuhi.
7 Ee Israeli, mtumaini Bwana,
maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma,
na kwake kuna ukombozi kamili.
8 Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli
kutoka dhambi zao zote.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 130: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha