Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 125

125
Zaburi 125
Usalama Wa Watu Wa Mungu
Wimbo wa kwenda juu.
1 Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni,
ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
2 Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,
ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake
sasa na hata milele.
3 Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi
waliopewa wenye haki,
ili wenye haki wasije wakatumia
mikono yao kutenda ubaya.
4 Ee Bwana, watendee mema walio wema,
wale walio wanyofu wa moyo.
5 Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,
Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya.
Amani iwe juu ya Israeli.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 125: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia