Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 12

12
Zaburi 12
Kuomba Msaada
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi.
1 Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;
waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo;
midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
3 Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila
na kila ulimi uliojaa majivuno,
4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda;
midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge
na kulia kwa uchungu kwa wahitaji,
nitainuka sasa,” asema Bwana.
“Nitawalinda kutokana na wale
wenye nia mbaya juu yao.”
6 Maneno ya Bwana ni safi,
kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,
iliyosafishwa mara saba.
7 Ee Bwana, utatuweka salama
na kutulinda na kizazi hiki milele.
8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali
wakati ambapo yule aliye mbaya sana
ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 12: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia