Zaburi 100
100
Zaburi 100
Dunia yote yaitwa kumsifu Mwenyezi Mungu
Zaburi ya shukrani.
1Mpigieni Mwenyezi Mungu kelele za shangwe, dunia yote.
2Mwabuduni Mwenyezi Mungu kwa furaha;
njooni mbele zake kwa nyimbo za shangwe.
3Jueni kwamba Mwenyezi Mungu ndiye Mungu.
Yeye ndiye alituumba, sisi tu mali yake;
sisi tu watu wake,
kondoo wa malisho yake.
4Ingieni malangoni mwake kwa shukrani
na katika nyua zake kwa kusifu,
mshukuruni yeye na kulisifu jina lake.
5Kwa maana Mwenyezi Mungu ni mwema
na fadhili zake zadumu milele;
uaminifu wake unadumu kwa vizazi vyote.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 100: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.