YouVersion Logo
Search Icon

Mathayo 9:27, 28, 29, 30, 31, 32, 33, 34, 35, 36, 37

Mathayo 9:27 NENO

Isa alipokuwa akiondoka mahali pale, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti na kusema, “Mwana wa Daudi, tuhurumie!”

Mathayo 9:28 NENO

Alipoingia mle nyumbani wale vipofu wakamjia. Naye Isa akawauliza, “Mnaamini kwamba ninaweza kufanya jambo hili?” Wakamjibu, “Ndiyo, Bwana.”

Mathayo 9:29 NENO

Ndipo Isa akagusa macho yao na kusema, “Iwe kwenu sawasawa na imani yenu.”

Mathayo 9:30 NENO

Macho yao yakafunguka. Isa akawaonya vikali, akisema, “Chungeni mtu yeyote asijue kuhusu jambo hili.”

Mathayo 9:31 NENO

Lakini wao wakaenda na kueneza habari zake katika eneo lile lote.

Mathayo 9:32 NENO

Walipokuwa wanatoka, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu na ambaye hakuweza kuongea aliletwa kwa Isa.

Mathayo 9:33 NENO

Yule pepo mchafu alipotolewa, yule mtu aliyekuwa bubu akaongea, na umati wa watu wakastaajabu na kusema, “Jambo kama hili kamwe halijapata kuonekana katika Israeli.”

Mathayo 9:34 NENO

Lakini Mafarisayo wakasema, “Huyo anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa mkuu wa pepo wachafu.”

Mathayo 9:35 NENO

Isa akazunguka katika miji yote na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri Habari Njema za ufalme, na akiponya kila ugonjwa na kila aina ya maradhi.

Mathayo 9:36 NENO

Alipoona umati wa watu, aliwahurumia kwa sababu walikuwa wanasumbuka bila msaada, kama kondoo wasiokuwa na mchungaji.

Mathayo 9:37 NENO

Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Mavuno ni mengi lakini watendakazi ni wachache.