Mathayo 3:1-3
Mathayo 3:1-3 NEN
Siku hizo Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Uyahudi, akisema, “Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni umekaribia.” Huyu ndiye yule aliyenenwa habari zake na nabii Isaya aliposema: “Sauti ya mtu aliaye huko nyikani, ‘Tayarisheni njia kwa ajili ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.’ ”