Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mathayo 22:35-40

Mathayo 22:35-40 NENO

Mmoja wao, mtaalamu wa Torati, akamuuliza swali ili kumjaribu, akisema, “Mwalimu, ni amri ipi katika Torati iliyo kuu kuliko zote?” Isa akamjibu, “ ‘Mpende Mwenyezi Mungu, Mungu wako, kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’ Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Nayo ya pili ni kama hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi yako.’ Amri hizi mbili ndizo msingi wa Torati na Manabii.”