Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Luka 7:11-17

Luka 7:11-17 NENO

Baadaye kidogo, Isa alienda katika mji mmoja ulioitwa Naini. Nao wanafunzi wake na umati mkubwa wa watu walienda pamoja naye. Alipokaribia lango la mji, alikutana na watu waliokuwa wamebeba maiti wakitoka nje ya mji. Huyu aliyekufa alikuwa mwana pekee wa mwanamke mjane. Umati mkubwa wa watu wa mji ule walikuwa pamoja na huyo mwanamke. Bwana Isa alipomwona yule mjane, moyo wake ulimhurumia, akamwambia, “Usilie.” Kisha akalikaribia jeneza, akaligusa. Nao wale waliokuwa wamelibeba wakasimama. Akasema, “Kijana, nakuambia, inuka.” Yule aliyekuwa amekufa akaketi akaanza kuongea, naye Isa akamkabidhi kwa mama yake. Watu wote wakajawa na hofu ya Mungu, nao wakamtukuza Mungu wakisema, “Nabii mkuu ametokea miongoni mwetu. Mungu amekuja kuwakomboa watu wake.” Habari hizi za mambo aliyoyafanya Isa zikaenea Yudea yote na sehemu zote za jirani.