Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yoshua 6:24-27

Yoshua 6:24-27 NEN

Kisha wakauchoma mji wote na kila kitu kilichokuwamo ndani yake. Lakini fedha, dhahabu, vyombo vya shaba na vya chuma wakaviweka katika hazina ya nyumba ya BWANA. Lakini Yoshua akamhifadhi Rahabu yule kahaba, jamaa yake yote na wote waliokuwa wa kwake, kwa sababu aliwaficha watu waliotumwa na Yoshua kuipeleleza Yeriko, naye anaishi miongoni mwa Waisraeli hata leo. Wakati ule Yoshua akatamka kiapo hiki akasema, “Aliyelaaniwa mbele za BWANA ni mtu atakayeinuka kuujenga tena mji huu wa Yeriko: “Kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza wa kiume ataiweka misingi yake; kwa gharama ya mtoto wake wa mwisho atayaweka malango yake.” Hivyo BWANA alikuwa pamoja na Yoshua, na sifa zake zikaenea katika nchi yote.