Ayubu 25
25
Bildadi anasema: Mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mwenyezi Mungu?
1Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu:
2“Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu;
yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.
3Je, majeshi yake yaweza kuhesabika?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
4Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?
5Ikiwa hata mwezi sio mwangavu
nazo nyota si safi machoni pake,
6sembuse mtu ambaye ni funza:
mwanadamu ambaye ni buu tu!”
Iliyochaguliwa sasa
Ayubu 25: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.