Isaya 40:27-31
Isaya 40:27-31 NEN
Kwa nini unasema, ee Yakobo, nanyi ee Israeli, kulalamika, “Njia yangu imefichwa BWANA asiione, Mungu wangu hajali shauri langu?” Je wewe, hufahamu? Je wewe, hujasikia? BWANA ni Mungu wa milele, Muumba wa miisho ya dunia. Hatachoka wala kulegea, wala hakuna hata mmoja awezaye kuupima ufahamu wake. Huwapa nguvu waliolegea na huongeza nguvu za wadhaifu. Hata vijana huchoka na kulegea, nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka, bali wale wamtumainio BWANA atafanya upya nguvu zao. Watapaa juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio wala hawatachoka, watatembea kwa miguu wala hawatazimia.