Isaya 25:7-9
Isaya 25:7-9 NEN
Juu ya mlima huu ataharibu sitara ihifadhiyo mataifa yote, kile kifuniko kifunikacho mataifa yote, yeye atameza mauti milele. BWANA Mwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote; ataondoa aibu ya watu wake duniani kote. BWANA amesema hili. Katika siku ile watasema, “Hakika huyu ndiye Mungu wetu; tulimtumaini, naye akatuokoa. Huyu ndiye BWANA, tuliyemtumaini; sisi tushangilie na kufurahia katika wokovu wake.”