Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 11:1-5

Isaya 11:1-5 NEN

Chipukizi litatokea kutoka shina la Yese, kutoka mizizi yake Tawi litazaa tunda. Roho wa BWANA atakaa juu yake, Roho wa hekima na wa ufahamu, Roho wa shauri na wa uweza, Roho wa maarifa na wa kumcha BWANA naye atafurahia kumcha BWANA. Hatahukumu kwa yale ayaonayo kwa macho yake, wala kuamua kwa yale ayasikiayo kwa masikio yake, bali kwa uadilifu atahukumu wahitaji, kwa haki ataamua wanyenyekevu wa dunia. Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, kwa pumzi ya midomo yake atawaua waovu. Haki itakuwa mkanda wake na uaminifu utakuwa mshipi kiunoni mwake.