Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 10:20-25

Isaya 10:20-25 NENO

Katika siku ile, mabaki ya Israeli, walionusurika wa nyumba ya Yakobo, hawatamtegemea tena yeye aliyewapiga, lakini watamtegemea kwa kweli Mwenyezi Mungu Aliye Mtakatifu wa Israeli. Mabaki watarudi, mabaki wa Yakobo watamrudia Mungu Mwenye Nguvu. Ingawa watu wako, ee Israeli, ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaorudi. Maangamizi yamekwisha amriwa, ni mengi tena ni haki. Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, atatekeleza maangamizi yaliyoamriwa juu ya nchi yote. Kwa hiyo, hili ndilo asemalo Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni: “Enyi watu wangu mnaoishi Sayuni, msiwaogope Waashuru, wanaowapiga ninyi kwa fimbo na kuinua rungu dhidi yenu, kama Misri ilivyofanya. Bado kitambo kidogo sana hasira yangu dhidi yenu itakoma, na ghadhabu yangu itaelekezwa kwenye maangamizi yao.”