Waebrania 10:35-39
Waebrania 10:35-39 NEN
Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kubwa mno. Inawapasa kuvumilia ili mkiisha kufanya mapenzi ya Mungu mpate kile alichoahidi. Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu, “Yeye ajaye atakuja wala hatakawia. Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Naye kama akisitasita, sina furaha naye.” Lakini sisi hatumo miongoni mwa hao wanaositasita na kuangamia, bali tuko miongoni mwa hao wenye imani na hivyo tunaokolewa.