Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Habakuki 3:7-13

Habakuki 3:7-13 NEN

Niliona watu wa Kushani katika dhiki, na makazi ya Midiani katika maumivu makali. Ee BWANA, uliikasirikia mito? Je, ghadhabu yako ilikuwa dhidi ya vijito? Je, ulighadhibikia bahari ulipoendesha farasi wako na magari yako ya ushindi? Uliufunua upinde wako na kuita mishale mingi. Uliigawa dunia kwa mito; milima ilikuona ikatetemeka. Mafuriko ya maji yakapita huko; vilindi vilinguruma na kuinua mawimbi yake juu. Jua na mwezi vilisimama kimya mbinguni katika mngʼao wa mishale yako inayoruka, na katika mngʼao wa mkuki wako umeremetao. Kwa ghadhabu ulipita juu ya dunia, na katika hasira ulikanyaga mataifa. Ulikuja kuwaokoa watu wako, kumwokoa uliyemtia mafuta. Ulimponda kiongozi wa nchi ya uovu, ukamvua toka kichwani hadi wayo.

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha