Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mwanzo 31:44-49

Mwanzo 31:44-49 NEN

Njoo sasa na tufanye agano, wewe na mimi, na liwe kama shahidi kati yetu.” Hivyo Yakobo akachukua jiwe, akalisimamisha kama nguzo. Akawaambia jamaa yake, “Kusanyeni mawe.” Hivyo wakachukua mawe na kuyakusanya yakawa lundo, wakala chakula hapo karibu na hilo lundo. Labani akaliita Yegar-Sahadutha na Yakobo akaliita Galeedi. Labani akasema, “Lundo hili ni shahidi kati yako na mimi leo.” Ndiyo maana likaitwa Galeedi. Pia liliitwa Mispa, kwa sababu alisema, “BWANA na aweke ulinzi kati yako na mimi wakati kila mmoja akiwa mbali na mwingine.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Mwanzo 31:44-49