Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kumbukumbu 26:16-19

Kumbukumbu 26:16-19 NEN

BWANA Mungu wako anakuagiza leo kufuata amri hizi na sheria; zishike kwa bidii kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote. Umetangaza leo kwamba BWANA ndiye Mungu wako na kwamba utafuata njia zake, kwamba utayashika maagizo yake, amri zake na sheria zake nawe utamtii. Naye BWANA ametangaza leo kwamba ninyi ni taifa lake, hazina yake ya thamani kama alivyoahidi, ili kwamba mpate kuyashika maagizo yake yote. Ametangaza kwamba atawaweka juu kuliko mataifa mengine aliyoyafanya katika sifa, kuwa fahari na heshima, na kwamba mtakuwa taifa takatifu kwa BWANA Mungu wenu, kama alivyoahidi.

Video for Kumbukumbu 26:16-19