Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Amosi 9:11-15

Amosi 9:11-15 NENO

“Katika siku ile “Nitalisimamisha hema la Daudi lililoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali, ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema BWANA ambaye atafanya mambo haya. “Siku zinakuja,” asema BWANA, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote. Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani yake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake. Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi niliyowapa,” asema BWANA Mungu wenu.