Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Wafalme Utangulizi

Utangulizi
Katika maandiko ya Kiebrania, vitabu vya 1 Wafalme na 2 Wafalme vilikuwa kitabu kimoja kilichoitwa “Wafalme” katika mapokeo ya Kiyahudi. Huku kutenganishwa kwa vitabu hivi kulifanywa na watafsiri wa Agano la Kale la Kiyunani “Septuagint” na kuvitambulisha kama “Kitabu cha Tatu na cha Nne cha Ufalme.” Vitabu vya Samweli na Wafalme vinaelezea historia yote kuhusu ufalme wa Israeli, vile ulivyoinuka wakati wa Samweli, na vile ulivyoanguka mikononi mwa Wababeli.
Mwandishi
Mwandishi wa kitabu hiki hajulikani, lakini mapokeo ya Kiyahudi yanasema mwandishi ni nabii Yeremia, au kikundi cha manabii.
Kusudi
Kulinganisha maisha ya wale waliomwishia Mungu na wale waliokataa kumwishia Mungu, kupitia historia ya wafalme wa Israeli na Yuda.
Mahali
Katika nchi ya Israeli.
Tarehe
Hakuna uhakika ni wakati upi hiki kitabu kiliandikwa.
Wahusika Wakuu
Daudi, Solomoni, Rehoboamu, Yeroboamu, Eliya, Ahabu na Yezebeli.
Wazo Kuu
Kugawanyika kwa Israeli kuwa falme mbili: Ufalme wa Kaskazini uliojulikana kama Israeli, ambao ulikuwa na makabila kumi, na Ufalme wa Kusini uliojulikana kama Yuda, ambao ulikuwa na makabila mawili.
Mambo Muhimu
Kifo cha Daudi, utawala wa Solomoni, kujengwa kwa Hekalu, kugawanyika kwa ufalme, na huduma ya Eliya.
Mgawanyo
Utawala wa Solomoni (1:1–11:43)
Rehoboamu na Yeroboamu (12:1–14:31)
Wafalme wa Israeli na Yuda (15:1–16:34)
Eliya na Ahabu (17:1–19:21)
Utawala wa Ahabu na Yezebeli (20:1–22:53).

Iliyochaguliwa sasa

1 Wafalme Utangulizi: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia