Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Wakorintho 10:1-10

1 Wakorintho 10:1-10 NEN

Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari. Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari. Wote walikula chakula kile kile cha roho, na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo. Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani. Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya. Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.” Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja. Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka. Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na 1 Wakorintho 10:1-10