Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Nyakati Utangulizi

Utangulizi
Jina hili la kitabu “Mambo ya Nyakati” linaweza likafuatiliwa hadi kwa Yerome ambaye alilitumia katika tafsiri ya Kilatini ya Neno la Mungu, yaani “Vulgate.” Jina la kitabu hiki katika Kiyunani, “Mambo Yaliyorukwa,” linaonyesha ile hali ya watafsiri wa Agano la Kale katika “Septuagint” kwamba mambo yaliyomo katika vitabu hivi kimsingi yalikuwa mambo ya nyongeza yaliyokuwa yameachwa na vitabu vya Samweli na Wafalme.
Vitabu vya 1 na 2 Mambo ya Nyakati viliandikwa kwa ajili ya watu waliorudi Israeli kutoka utumwani, baada ya kutekwa na kupelekwa Babeli, ili kuwakumbusha kwamba walikuwa wa ukoo wa ufalme wa Daudi, na kwamba wao walikuwa watu wateule wa Mungu.
Mwandishi
Mapokeo ya Kiyahudi husema ni Ezra.
Kusudi
Kuunganisha watu wa Mungu, kufuatilia ukoo wa Daudi, na kufundisha watu sala iliyo ya kweli ambayo ndiyo hitaji kubwa katika maisha ya mtu binafsi na taifa pia.
Mahali
Yerusalemu, na katika Hekalu.
Tarehe
Kama mwaka wa 430 K.K.
Wahusika Wakuu
Daudi na Solomoni.
Wazo Kuu
Kitabu cha 1 Mambo ya Nyakati kinaelezea kwa kifupi historia na koo za Waisraeli tangu Adamu hadi kifo cha Mfalme Sauli. Sehemu ya kitabu iliyobaki inaeleza habari za Mfalme Daudi.
Mambo Muhimu
Kuelezea historia ya vizazi vya Israeli, na habari kumhusu Mfalme Daudi na uhusiano wake na Mungu, na kuletwa kwa Sanduku la Agano huko Yerusalemu kama chanzo cha sala ya kweli.
Mgawanyo
ORODHA YA VIZAZI (1:1–9:44)
1. Orodha ya nasaba za mababa wa taifa
2. Makabila ya Israeli
3. Kurudi kutoka utumwa Babeli.
UTAWALA WA DAUDI (10:1–29:30)
1. Daudi afanyika mfalme juu ya Israeli yote
2. Daudi alirudisha Sanduku la Bwana Yerusalemu
3. Majeshi ya Daudi yajinufaisha
4. Daudi aandaa kwa ajili ya ujenzi wa Hekalu.

Iliyochaguliwa sasa

1 Nyakati Utangulizi: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha