1
Mhubiri 3:1
Swahili Revised Union Version
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.
Linganisha
Chunguza Mhubiri 3:1
2
Mhubiri 3:2-3
Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa kilichopandwa; Wakati wa kuua, na wakati wa kuponya; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga
Chunguza Mhubiri 3:2-3
3
Mhubiri 3:4-5
Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza; Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia
Chunguza Mhubiri 3:4-5
4
Mhubiri 3:7-8
Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena; Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.
Chunguza Mhubiri 3:7-8
5
Mhubiri 3:6
Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa
Chunguza Mhubiri 3:6
6
Mhubiri 3:14
Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye.
Chunguza Mhubiri 3:14
7
Mhubiri 3:17
Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki; kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi.
Chunguza Mhubiri 3:17
Nyumbani
Bibilia
Mipango
Video