“Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli,
nirudie mimi,”
asema Mwenyezi Mungu.
“Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu
na usiendelee kutangatanga,
ikiwa utaapa katika kweli, kwa haki na kwa unyofu,
‘Hakika kama Mwenyezi Mungu aishivyo,’
ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye,
na ndani yake watajitukuza.”