1
Mwanzo 42:21
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
Wakaambiana wao kwa wao, “Hakika tunaadhibiwa kwa sababu ya ndugu yetu. Tuliona jinsi alivyohuzunika alipokuwa anatusihi kuokoa maisha yake, lakini hatukumsikiliza. Hiyo ndiyo sababu dhiki hii imetupata.”
Linganisha
Chunguza Mwanzo 42:21
2
Mwanzo 42:6
Wakati huo Yusufu alikuwa mtawala wa nchi ya Misri, na ndiye aliwauzia watu wote nafaka. Kwa hiyo wakati ndugu zake Yusufu walifika, wakamsujudia hadi nyuso zao zikagusa ardhi.
Chunguza Mwanzo 42:6
3
Mwanzo 42:7
Mara Yusufu alipowaona ndugu zake, akawatambua. Lakini akajifanya mgeni na kuzungumza nao kwa ukali, akiwauliza, “Ninyi mnatoka wapi?” Wakamjibu, “Tumetoka nchi ya Kanaani kuja kununua chakula.”
Chunguza Mwanzo 42:7
Nyumbani
Bibilia
Mipango
Video