Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Flp 4:7

Ondoa uoga
Siku 3
Unaweza kushinda hisia za uoga. Dk. Tony Evans anakuongoza kwenye njia ya uhuru katika mpango huu maalum. Vumbua maisha ya furaha na amani ambayo umekuwa ukiyasubiri unapotumia kanuni zinazoletwa na mpango huu

Bila Utulivu
Siku 3
"Mioyo yetu haina utulivu mpaka ipate ulivu kwako." Haijawahi kutokea kuwa wengi wetu tukakosa utulivu Agustine alielezea kwa hii sentesi maarufu. Lakini suluhisho kwa kukosa utulivu wa kweli kwetu ni nini? Huu mpango wa siku tatu utakuonesha, suluhisho kwa sehemu katika kuona vitendo vya kale vya sabato kwa lenzi tofauti ya "wewe" -- Yesu ndie mwanzo wa amani.

Fukuza Hofu
Siku 3
Unaweza kushinda hisia za hofu. Dkt. Tony Evans anakuongoza kwenye njia ya uhuru katika mpango huu wa usomaji wa kupata ufahamu. Gundua maisha ya furaha na amani ambayo umekuwa ukitaka, unapotumia kanuni zilizowekwa katika mpango huu.

Kupata Uhuru kutokana na Kufadhaika
Siku 5
Kufadhaika huwa, lakini hakufai kuyaendesha maisha yako. Kumpitia Kristo, tunaweza kuibadilisha, kuiona upya na kuitafsiri upya. Kama unapata changamoto na kufadhaika, angalia mpango huu wa Bibilia wa siku 5 ili ujifunze kupata uhuru na amani.

Kuanza: Mwongozo Rahisi Wa Kuomba Kwa Ujasiri
Siku 6
Maombi ni zawadi, fursa nzuri ya kuwa na uhusiano na Baba yetu wa Mbinguni. Katika mpango huu wa siku 6, tutatambua yale ambayo Yesu alitufundisha kuhusu maombi na kuhimizwa kuomba kwa mfululizo na ujasiri mkubwa.

Kufuata Amani
Siku 7
Tearfund inatafuta uongozi wa Mungu ili iwe sauti ya nguvu juu ya amani, mahusiano kurudishwa, na upatanifu kati ya jumuiya mbalimbali katika dunia. Somo hili la siku 7 lina matendo ya kila siku ili urudishe mahusiano yako na wengine na uombee dunia tunayoishi. Somo hili linatumia hekima kutoka methali za Afrika kutusaidia kufunua amani ya kweli ya Mungu.

Usijisumbue kwa Lolote
siku 7
Ingekuwaje kama kungekuwa na njia bora ya kupigana na hofu isiyoisha inayokufanya kukosa usingizi? Pumziko halisi lipo--yawekana karibu zaidi ya unavyofikiria. Badilisha hofu na amani kupitia siku hizi 7 za mpango wa Biblia kutoka Life.Church, ikiambatana na mfululizo wa ujumbe wa Mchungaji Craig Groeschel Usijisumbue kwa Lolote.

Kwa pamoja: Kutafuta maisha pamoja
Siku 7
Unapofikia umri wa miaka 18, unaanza kuona kwamba unahitaji kupanga maisha yako. Itakuwaje usipofanya hivyo? Itakuwa kama ulipofikiria utakuwa sipo ulipo sasa? Hauko peke yako. Hebu tuangalie swali kuu la maisha yetu pamoja katika mpango huu wa Biblia wa siku 7 kwa pamoja, mafunzo ya vijana kutoka Life. Church.

Maombi Hatari
Siku 7
Umechoka kujali usalama katika imani yako? Uko tayari kukabili hofu zako, kujenga imani yako, na kufikia uwezo wako kamili? Mpango huu wa Biblia wa siku 7 kutoka kwenye kitabu cha Mchungaji Craig Groeschel wa Life.Church, "Dangerous Prayers" yaani Maombi Hatari, unakujasiri uombe bila kujali usalama—kwa sababu kumfuata Yesu haukufaa kuwa salama salmini.

Acha! Usiwe Na Wasiwasi Zaidi
Siku 7
Je! unajua Yesu anasema nini kuhusu wasiwasi wetu? Acha. Ndiyo, anatuambia tuiache. Wasiwasi ni moja ya dalili kuu kwamba imani yetu imetikisika na imani yetu iko chini. Wakati wewe au mimi tunakuwa na wasiwasi, tunakosa kuweka imani ifaayo juu ya udhibiti mkuu wa Mungu. Bado sote, bado tunafanya hivyo, sivyo? Ndiyo maana Tony Evans ameweka pamoja mpango wa kusoma wa siku 7 ili kukusaidia WEWE kushinda wasiwasi. Unaweza kuvunja mzunguko na kubadilishana wasiwasi kwa amani.

Mzabibu
12 Siku
Moja ya maswali ya kawaida kwa watu ambao ni wapya katika kumfuata Yesu ni, “Nifanye nini sasa?” Ina maana gani kumpenda, kumtii, na kuwa sehemu ya jamii ya waumini? Mpango huu wa usomaji unatoa mfumo wa kibiblia wa jinsi ya kuunganisha uhusiano wako wa kibinafsi na Yesu na utume wa kanisa.

Kuwa Karibu Na Mungu Kila Siku
Siku 14
Katika mpango huu wa ibada ya Siku 14 Joyce husaidia wasomaji kufikia maisha ya ujasiri zaidi, yenye furaha kwa kukua karibu katika uhusiano wao na Mungu.

Kutafuta Amani
Siku 10
Unataka amani zaidi katika maisha yako? Unataka utulivu uwe zaidi ya matamanio yako? Unaweza kupata amani kutoka kwenye chanzo kimoja tuu--Mungu. Jiunge na Dkt. Charles Stanley anapokuonesha njia ya kubadilisha amani ya mawazo yako, akikupa nyenzo za kutatua majuto yaliyopita, kukabiliana na wasiwasi wa sasa, na kutuliza wasiwasi wa mambo yajayo.

BibleProject | Tafakari ya Ujio wa Yesu
Siku 28
BibleProject ilibuni Tafakari ya Ujio wa Yesu ili kuhamasisha watu mmoja mmoja, vikundi vidogo vidogo, na familia kusherehekea majilio, au kuwasili kwa Yesu. Mwongozo huu wa wiki nne unashirikisha video za kikatuni, mihutasari mifupi, na maswali ya kutafakari ili kuwasaidia washiriki kuchunguza maana ya Biblia ya tumaini, amani, furaha, na upendo. Chagua mwongozo huu ili kujifunza jinsi maadili haya manne yamefika ulimwenguni kupitia kwa Yesu.

Oswald Chambers: Amani - Maisha kwenye Roho
Siku 30
Amani: Maisha ya Roho ni hazina ya msukumo ya nukuu kutoka kwenye kazi za Oswald Chambers, mwandishi mpendwa ulimwenguni wa ibada na mwandishi wa My Utmost for His Highest. Pata mapumziko kwa Mungu na pata uelewa zaidi wa umuhimu wa amani ya Mungu kwenye maisha yako.

Ahadi za kila siku ya maisha yako
30 Siku
Mungu ametupa ahadi tele ambazo tunahitaji kutembea ndani yake. Lakini ni muhimu kuzijua, kuziamini ili tuweze kuziona zikidhirika maishani mwetu. Kila siku, kuna ahadi kwa ajili yako. Unapoanza siku yako, pata kufahamu ahadi hizi!

Soma Biblia Kila Siku Juni/2022
Siku 30
Soma Biblia Kila Siku Juni/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Juni pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Wafilipi na Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure

Jolt ya Furaha
Siku 31
Biblia inatuambia kwamba "Katika uwepo wake kuna furaha tele" na kuwa "furaha ya Bwana ni nguvu yetu". Furaha sio hisia tu bali ni tunda la Roho na mojawapo ya silaha bora katika gala letu la kupigana na kuvunjika moyo, huzuni na kushindwa. Tumia siku 31 ukijifunza ni nini Biblia inasema kuhusu Furaha na kujiimarisha kuwa Mkristo mwenye Furaha bila wasi wasi.