Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Flp 2:8

Kupata Uhuru kutokana na Kufadhaika
Siku 5
Kufadhaika huwa, lakini hakufai kuyaendesha maisha yako. Kumpitia Kristo, tunaweza kuibadilisha, kuiona upya na kuitafsiri upya. Kama unapata changamoto na kufadhaika, angalia mpango huu wa Bibilia wa siku 5 ili ujifunze kupata uhuru na amani.

Kukua katika Upendo
Siku 5
Kinachojalisha kwa kweli ni kumpenda Mungu na kuwapenda wengine, lakini tunawapendaje kwa ufanisi? Ukweli ni kwamba, hatuwezi kuwapenda watu vizuri kwa nguvu zetu wenyewe. Lakini tunapomuangalia Mungu na kunyenyekea, tunaweza kuishi katika nguvu kamili ya upendo wa Mungu. Jifunze zaidi kuhusu kukua katika upendo katika mpango wa siku 5 kutoka wa Mchungaji Amy Groeschel.

Mwanamume Wa Kifalme
Siku 5
Katika historia yote, Mungu daima amewatafuta na kuwatumia wanaume kuendeleza ajenda ya Ufalme wake. Shetani anajua hili, ndiyo maana anataka kuwafungia na kuwahasi wanaume. Ulimwengu wetu unaendelea ukizorota kwa sababu wanaume hawapatikani popote. Ni wakati wa wanaume kusimama kidete. Katika mpango huu wa kusoma wa siku tano, Daktari Tony Evans atakupeleka kwenye safari ya kufanyika mwanamume ambaye Mungu alikuumba uwe.

Yesu Ananipenda
Siku 7
Ikiwa mtu angekuuliza, "Ninahitaji kuamini ipi ili niwe Mkristo?" ungemjibu vipi? Kwa kutumia maneno ya wimbo upendwao, "Yesu anipenda, kweli ninajua, kwani Biblia inasema”, mhubiri aliyekuwa mwanahabari anakusaidia kuelewa unachoamini na sababu. Mwandishi maarufu John S. Dickerson anafafanua imani za kimsingi za Kikristo kwa uwazi na uaminifu na kuashiria mbona imani hizi ni muhimu.

Msalaba Na Pasaka
Siku 7
Tunavaa misalaba shingoni mwetu, lakini tunapaswa kuitumiaje kwa maisha yetu? Kazi ya Yesu ina nguvu ya ajabu kwetu. Bila Ijumaa, hakungekuwa na Jumapili. Pasaka isingetokea bila msalaba. Gundua jinsi msalaba unavyounganamanisha katika maisha yako kupitia mpango huu wa usomaji wa ibada unapotayarisha moyo wako kwa Pasaka.

Mzabibu
12 Siku
Moja ya maswali ya kawaida kwa watu ambao ni wapya katika kumfuata Yesu ni, “Nifanye nini sasa?” Ina maana gani kumpenda, kumtii, na kuwa sehemu ya jamii ya waumini? Mpango huu wa usomaji unatoa mfumo wa kibiblia wa jinsi ya kuunganisha uhusiano wako wa kibinafsi na Yesu na utume wa kanisa.

Soma Biblia Kila Siku Juni/2022
Siku 30
Soma Biblia Kila Siku Juni/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Juni pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Wafilipi na Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure